Tuesday, 12 January 2016
Assalamu Alaykum warahmatullahi taala Wabarakatuhu.leo tujifunze somo la kwanini yawepo maradhi.mwenyezmungu anasema katika kitabu chake kitukufu. "na kwa Hakika tutawajaribu kwa jambo la khofu na njaa na upungufu wa wa mali na nafsi na matunda, nawe wape habari ya furaha wenye kusubiri. Ambao ukiwafika msiba, husema :Hakika sisi ni wa mwenyezimungu na sisi tu wenye kurejea kwake. Hao juu yao ziko baraka na rehema kutoka kwa mola wao, nao ndio wenye kuongoka (baqara:155-157)aya hiyo inaeleza suala la majaribu ya mwenyezimungu kwa waja wake katika nyanja mbali mbali, kwa mujibu wa Aya hiyo tukufu tunaelezwa kuwa nusura hapatikani kwa njia yeyote ispokuwa chini ya kivuli cha subira na kutawakali kwa mwenyezimungu.kwahiyo yanakuwepo maradhi kwa ajiri ya mwenyezimungu kuwajaribu waja wake . inshaallah tutaendelea.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment